AFA NA KUZINDUKA

Familia moja nchini India iliyokuwa ikiomboleza kifo cha ndugu yao, ilipatwa na mshangao na hali ya furaha baada ya ndugu yao huyo kuzinduka.
Mke wa bwana huyo pamoja na jamaa zake walikuwa wakibubujikwa na machozi kwa kifo cha ghafla cha Vijay Kumar Ratre mwenye umri wa miaka 32, ambaye alikutwa akielea katika dimwi la maji kwa muda mrefu.
Mtandao wa Indo Asia news umesema polisi wa eneo hilo la Raipur walifika na kuuopoa mwili wa bwana huyo, huku kundi la karibu watu mia moja likiwa limekusanyika kuomboleza. Polisi waliita gari la kubebea wagonjwa ili mwili ufanyiwe uchunguzi kabla ya kwenda kuzikwa.
Mara tu mwili huo ulipowekwa ndani ya gari, bwana Vijay alizinduka na kujaribu kuruka na kutoka ndani ya gari. Umati wa watu uliokusanyika ulilipuka kwa furaha baada ya kuona tukio hilo. Polisi wamesema bwana huyo alikuwa amelewa chakari bila hata kujua kilichokuwa kikitokea.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI