MAREKANI HATIMAYE KUTETA NA TALEBANI

Alipohojiwa na BBC, kabla ya kuanza ziara yake Uingereza Jumatatu, Rais Obama ameonesha kuwa atakuwa tayari kuamrisha operesheni nchini Pakistan, dhidi ya kiongozi mwengine wa Al Qaeda au Taliban.

Ingawa Rais Obama alisema yuko tayari kuchukua hatua dhidi ya Mullar Omar kiongozi wa Taliban, lakini kauli yake ilikuwa tafauti kuhusu vita dhidi ya Taliban nchini Afghanistan.
Alifahamisha wazi kuwa vita virefu kabisa vya Marekani vinaweza kumalizika kwa mazungumzo na adui:
"Hatuwezi kumaliza tatizo hili kwa vita.
Tunachoweza kufanya ni kutumia mafanikio tuliyopata kijeshi kutafuta suluhisho la kisiasa.
Inamaanisha kuwa hatimaye lazima tuzungumze na Taliban, ingawa tumeweka shuruti kabla ya mazungumzo ya maana kufanyika.
Taliban lazima ikate uhusiano na Al Qaeda, iache kutumia nguvu, na itabidi iheshimu katiba ya Afghanistan."

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.