NKOROMO AMRITHI MWAIKENDA UPIGA PICHA BORA TANZANIA






MENEJA Mipango wa Mfuko wa Ruzuku kwa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF)
Ernest Sungura (kushoto) akimkabidhi tuzo ya mpigapicha bora wa picha za habari,
Mpigapicha Mwandamizi wa Kampuni ya Uhuru Publicatiosn Ltd, Bashir Nkoromo,
baada ya kushinda tuzo hiyo, katika hafla ya utoaji Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa
Habari (EJAT), jana, katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Mtayarishaji Mkuu wa Blogu hii, ambaye ni mpigapicha wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, Bashir Nkoromo, ameng'ara katika Tuzo ya Umahiri ya Uandishi wa Habari (EJAT) kwa mwaka 2010.
Nkoromo aliibuka mshindi wa picha bora dhidi ya Mpigapicha wa magazeti ya Daily News na Habari Leo, Robert Okanda, na kukabidhiwa tuzo, cheti na zawadi ya kamera.
Katika hafla hiyo iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, Mhariri wa Habari wa Uhuru FM, Pius Ntiga, alipata Tuzo ya Elimu akimshinda Adeladius Makwega wa TBC Taifa.
Akishukuru baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Nkoromo alisema kwamba ushindi wake haumaanishi kuwa yeye ni bora zaidi ya wapigapicha wengine katika vyombo vya habari, bali picha aliyoipiga ambayo imempatia ushindi ndiyo ilikuwa bora.


Wadau mbalimbali wa sekta ya habari walihudhuria hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa, Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta.


Tuzo nyingine kadhaa zilikwenda kwa waandishi wa habari, watangazaji wa redio, televisheni na wachoraji wa katuni wa vyombo mbalimbali vya habari.


Akizungumza kweye hafla hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania (MCT), Kajubi Mkajanja,alisema utozji tuzo hizo umefikiwa baada ya kupata wateule 76, kupitia na kuchuja kazi 437 zilizowasilishwa na waandishi mbalimbali wa habari katika makundi 16 ya tuzo zinazoshindaniwa.

NB
Richard Mwaikenda ambaye ni mtayarishaji wa Blogu hii, alikuwa Mpiga Picha Bora 2009. Nachukua fursa hii kumpongeza Bashir Nkoromo kwa kutwaa tuzo hii kwa mwaka 2010.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.