Polisi nchini Marekani wamemkamata na kumshitaki bwana mmoja kwa kutumia vibaya namba ya simu ya dharura
Mtandao wa cnews.com umesema polisi walimshitaki Bwana Raymond Roberge mwenye umri wa miaka 65, kwa kupiga simu hiyo, namba 911.
Bwana huyo alipiga simu hiyo na kusema amepatwa na dharura, na alipoulizwa dharura gani, alijibu kuwa ameishiwa bia alizokuwa anakunywa. Taarifa zinasema bwana huyo wa mjini Bridgeport, Connecticut, alipiga simu mara tatu, akiomba kutatuliwa dharura yake hiyo.
Gazeti la Connecticut Post pia limeripoti kuwa hii si mara ya kwanza kwa Bwana Raymond kufanya hivyo, kwani amekwishawahi kupiga simu huyo pasipo na dharura rasmi, takriban mara themanini.
Mtandao wa cnews.com umesema polisi walimshitaki Bwana Raymond Roberge mwenye umri wa miaka 65, kwa kupiga simu hiyo, namba 911.
Bwana huyo alipiga simu hiyo na kusema amepatwa na dharura, na alipoulizwa dharura gani, alijibu kuwa ameishiwa bia alizokuwa anakunywa. Taarifa zinasema bwana huyo wa mjini Bridgeport, Connecticut, alipiga simu mara tatu, akiomba kutatuliwa dharura yake hiyo.
Gazeti la Connecticut Post pia limeripoti kuwa hii si mara ya kwanza kwa Bwana Raymond kufanya hivyo, kwani amekwishawahi kupiga simu huyo pasipo na dharura rasmi, takriban mara themanini.
Comments