Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Mh. Mwankenja ameuawa kwa kupigwa risasi usiku wa leo majira ya Nne na dk 10 nyumbani kwake Kiwira. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa marehemu Mwankenja alipigwa risasi akiwa ndani ya gari lake mara baada ya kuwasili nyumbani kwake.
Wauaji walitoweka mara baada ya kukamilisha mauaji yao na kabla ya watu kukusanyika. Hadi sasa sababu za mauaji hayo hazijafahamika. Hata hivyo baadhi ya viongozi waliofika nyumbani kwa marehemu usiku huu wanahofu mauaji hayo kuhusiana na masuala ya kisiasa.
Wauaji walitoweka mara baada ya kukamilisha mauaji yao na kabla ya watu kukusanyika. Hadi sasa sababu za mauaji hayo hazijafahamika. Hata hivyo baadhi ya viongozi waliofika nyumbani kwa marehemu usiku huu wanahofu mauaji hayo kuhusiana na masuala ya kisiasa.
Comments