NATO YAISHAMBULIA LIBYA USIKU KUCHA

Takriban milipuko mikubwa mitano imeitikisa Tripoli usiku kucha, wakati harakati za majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato zikiendelea kwenye mji mkuu wa Libya.
Kwa usiku wa pili, mashambulio ya anga yalilenga ngome ya Bab al-Aziziya ya Kanali Muammar Gaddafi.
Nato inatekeleza azimio la umoja wa mataifa la kulinda raia wa Libya, kufuatia maandamano dhidi ya uongozi wa Kanali Gaddafi.
Lakini Urusi, ambayo haikuunga mkono azimio hilo, imesema uvamizi huo ni ukiukwaji wa umoja huo.
Mwandishi wa BBC Andrew North mjini Tripoli alisema mashambulio ya Jumanne usiku si makubwa kama yaliyofanyika Jumatatu usiku, lakini bado yalitikisa majengo eneo kubwa.
Moshi ulionekana kutanda kwenye mji huo.
Nato ilisema ngome hiyo ya Bab al-Aziziya imekuwa ikitumika kama kituo cha majeshi na magari ya kijeshi yaliyotumika kushambulia raia.
Lakini serikali ya Libya imesema Nato inajaribu kumwuua Kanali Gaddafi na mashambulio ya usiku yanawatisha raia wa Tripoli.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.