Ofisa Uhusiano wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mwanakombo Mohamed akigawa mfuko wenye fulana, kofia na vijarida vya NSSF kwa wanachama wa kikundi cha wajasiriamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, waliohudhuria semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, Dar es Salaam
Mwanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Editha Rimoy akisoma kijarida cha mafao ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), alichopewa wakati wa semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, Dar es Salaam juzi.
Mwanachama Hidaya Mohamed wa kikundi cha wajasiriamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, akiuliza swali kwa mwendesha mada, Chritene Kamuzora (kutoka) kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakati wa semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, Dar es Salaam juzi.
Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chritine Kamuzora (kulia), akielezea faida ya kujiunga na mfuko huo katika semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, iliyowahusisha wanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapinda.
Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chritine Kamuzora (kulia), akielezea faida ya kujiunga na mfuko huo katika semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, iliyowahusisha wanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapinda.
Na Mwandishi Wetu
WAJASIRIAMALI wamekunwa na mpango wa Mfuko wa
Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wa kuwapatia
mafao ya mishahara ya miezi mitatu
Wanawake wanachama wao wanaojifungua.
Wajasiriamali wa Kikundi cha Muungano wa
Wanawake wa Sekta isiyo rasmi Dar es Salaam
(MUWASIDA SACCOS) waliufurahia mpango huo
ulioelezwa, Dar es Salaam juzi, na Ofisa
Matekelezo Mwandamizi wa NSSF, Christine Kamuzora
katika semina ya siku moja ya elimu ya umma
kuhusu faida lukuki anazoweza kuzipata mwanachama
wa mfuko huo.
Alisema kuwa licha ya Mwanamke mjamzito kupata
mafao lakini vile vile hunufaika zaidi kwa NNS
kumpatia jumla ya mishahara miezi mitatu
anapojifungua ili imsaidie wakati wa kulea mtoto.
Kamuzora alisema kiwango cha mshahara kinatolewa
kulingana ama zaidi ya mshahara unaotolewa na
mwajiri wa mwanachama huyo.
Alisema, mpango maalumu unaandaliwa kwa
wajasiriamali wa kujitolea ambao si wafanyakazi
ili nao wanufaike na mpango huo pamoja na mafao
mengine yatolewayo na mfuko huo.
Pia Kamuzora, alitumia fursa hiyo kuwaeleza
wajasiriamali hao, kuhusu umuhimu wa kujiunga na
mfuko huo ili wanufaike na mafao mbalimbali
yanayotolewa kwa wanachama.
Alitaja mafao hayo kuwa ni; Pensheni ya uzeeni,
Pensheni ya Ulemavu, Pensheni ya Urithi,mafao ya
Matibabu,Mafao ya Uzazi,Mafao ya Kuumia Kazini na
Mafao ya Mazishi.
Aliwaeleza kuwa katika Mafao ya Matibabu
wanachama wajasriamali hunufaika kwa kupatiwa
huduma ya tiba bure kwa miezi mitatu hata akiacha
kuchangia mfuko ambao ni asilimia 20 ya mshahara
ama kipato anachopata katika biashara zake.Lakini
kwa wafanyakazi waliochangia muda mrefu hunufaika
kwa kupatiwa tiba bure hadi kifo chake.
Alisema huduma hiyo ambayo hupatikana katika
hospitali walizoingia nazo mkataba, hutolewa bila
ubaguzi kwani kila mwanachama ana haki hiyo na
kwamba hawana madaraja ya juu, kati wala ya
chini.Wanaonufaika katika mpango huo kifamilia ni
Baba, Mama na Watoto wanne.
Kamuzora alitoa mwito kwa wajasiriamali kujiunga
kwa wingi ili wanufaike na mafao hayo na
kusisitiza kuwa wasiwe na hofu yoyote kwani NSSF
imesimama imara hata vitukuu vyao wataikuta,
haitetereki kwa upepo, kimbunga wala Tsunami.
Mwanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Editha Rimoy akisoma kijarida cha mafao ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), alichopewa wakati wa semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, Dar es Salaam juzi.
Mwanachama Hidaya Mohamed wa kikundi cha wajasiriamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, akiuliza swali kwa mwendesha mada, Chritene Kamuzora (kutoka) kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakati wa semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, Dar es Salaam juzi.
Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chritine Kamuzora (kulia), akielezea faida ya kujiunga na mfuko huo katika semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, iliyowahusisha wanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapinda.
Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chritine Kamuzora (kulia), akielezea faida ya kujiunga na mfuko huo katika semina ya elimu ya umma kuhusu mfuko huo, iliyowahusisha wanachama wa kikundi cha wajasiliamali cha akina mama wa Ubungo cha MUWASIDA Saccos, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapinda.
Na Mwandishi Wetu
WAJASIRIAMALI wamekunwa na mpango wa Mfuko wa
Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wa kuwapatia
mafao ya mishahara ya miezi mitatu
Wanawake wanachama wao wanaojifungua.
Wajasiriamali wa Kikundi cha Muungano wa
Wanawake wa Sekta isiyo rasmi Dar es Salaam
(MUWASIDA SACCOS) waliufurahia mpango huo
ulioelezwa, Dar es Salaam juzi, na Ofisa
Matekelezo Mwandamizi wa NSSF, Christine Kamuzora
katika semina ya siku moja ya elimu ya umma
kuhusu faida lukuki anazoweza kuzipata mwanachama
wa mfuko huo.
Alisema kuwa licha ya Mwanamke mjamzito kupata
mafao lakini vile vile hunufaika zaidi kwa NNS
kumpatia jumla ya mishahara miezi mitatu
anapojifungua ili imsaidie wakati wa kulea mtoto.
Kamuzora alisema kiwango cha mshahara kinatolewa
kulingana ama zaidi ya mshahara unaotolewa na
mwajiri wa mwanachama huyo.
Alisema, mpango maalumu unaandaliwa kwa
wajasiriamali wa kujitolea ambao si wafanyakazi
ili nao wanufaike na mpango huo pamoja na mafao
mengine yatolewayo na mfuko huo.
Pia Kamuzora, alitumia fursa hiyo kuwaeleza
wajasiriamali hao, kuhusu umuhimu wa kujiunga na
mfuko huo ili wanufaike na mafao mbalimbali
yanayotolewa kwa wanachama.
Alitaja mafao hayo kuwa ni; Pensheni ya uzeeni,
Pensheni ya Ulemavu, Pensheni ya Urithi,mafao ya
Matibabu,Mafao ya Uzazi,Mafao ya Kuumia Kazini na
Mafao ya Mazishi.
Aliwaeleza kuwa katika Mafao ya Matibabu
wanachama wajasriamali hunufaika kwa kupatiwa
huduma ya tiba bure kwa miezi mitatu hata akiacha
kuchangia mfuko ambao ni asilimia 20 ya mshahara
ama kipato anachopata katika biashara zake.Lakini
kwa wafanyakazi waliochangia muda mrefu hunufaika
kwa kupatiwa tiba bure hadi kifo chake.
Alisema huduma hiyo ambayo hupatikana katika
hospitali walizoingia nazo mkataba, hutolewa bila
ubaguzi kwani kila mwanachama ana haki hiyo na
kwamba hawana madaraja ya juu, kati wala ya
chini.Wanaonufaika katika mpango huo kifamilia ni
Baba, Mama na Watoto wanne.
Kamuzora alitoa mwito kwa wajasiriamali kujiunga
kwa wingi ili wanufaike na mafao hayo na
kusisitiza kuwa wasiwe na hofu yoyote kwani NSSF
imesimama imara hata vitukuu vyao wataikuta,
haitetereki kwa upepo, kimbunga wala Tsunami.
Comments