UJERUMANI KUTEKETEZA VINU VYA NYUKLIA

Kufuatia mazungumzo ya usiku kutwa ya serikali ya mseto nchini Ujerumani, nchi hiyo imetangaza kubadilisha sera kuhusiana na nguvu za nuklia.
Ujerumani imetangaza kwamba itakomesha utumizi wa vinu 17 vya nguvu za nuklia kufikia mwaka 2022.
Uamuzi huo unaifanya Ujerumani kuwa taifa la kwanza kubwa ambalo limeendelea sana kiviwanda kutangaza kutupilia mbali utumizi wa nguvu za nuklia.
Mataifa kadhaa yamekuwa yakizichunguza sera zake kuhusiana na nguvu za nuklia, hasa kufuatia janga la Fukushima nchini Japan, mwezi Machi.
Nchi ya Uswisi wiki iliyopita ilikuwa nchi ya kwanza ya Ulaya kutangaza kwamba itasimamisha utumizi wa nguvu za nuklia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA