UN YAISIHI UGANDA

Afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na haki za kibinaadamu, Navi Pillay, ameisihi Uganda kuacha kutumia kile alichokielezea kuwa nguvu nyingi dhidi ya waandamanaji wa upinzani.

Bibi Pillay alisema hatua za wakuu wa Uganda ndio sababu kubwa iliyogeuza maandamano ya amani kuwa msuko-suko wa kitaifa, ambapo watu kama wanane waliuwawa.
Afisa huyo wa Umoja wa Mataifa alisema aliyotendewa kiongozi wa upinzani, Dakta Kizza Besigye, yameshtuwa.
Bwana Besigye bado hawezi kuona sawa sawa, baada ya kurushiwa pilipili machoni, na polisi wa Uganda.
Maandamano mengine ya kupinga kuzidi kwa gharama za maisha, yanapangwa kufanywa Jumatatu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA