VIJANA WAANDAMANA HISPANIA



Maelfu ya waandamanaji wamekesha katika medani ya kati ya mji wa Madrid ingawa mkusanyiko huo umepigwa marufuku na tume ya uchaguzi, kwa sababu ya uchaguzi wa majimbo wa hapo kesho.

Wimbi hilo la maandamano lilianza siku 6 zilizopita, na kusambaa katika miji kadha ya Uspania.
Maandamano yanaongozwa na vijana waliochoka na ukosefu wa ajira, ambao umefikia asli-mia-45% kati ya vijana, na rushwa na hisia kuwa wanasiasa hawawakilishi wao.
Mamia wameikalia medani ya Puerta del Sol kila siku, na wengine maelfu wanajumuika nao usiku.
Polisi wanasema waandamanaji elfu 25 walijaa katika medani na kufurika katika barabara za kando kando.
Saa sita za jana usiku, wakati amri ya kupiga marufuku maandamano hayo ilipoanza, umati huo ulikaa kimya kwa dakika, kisha ukaripuka kwa zomeo na kelele.
Tume ya uchaguzi ya Uspania ilitoa amri kuwa watu watawanyike jana usiku ili, "watu wapate muda wa kutafakari", kabla ya uchaguzi wa majimbo na serikali za mitaa utaofanywa kesho.
Lakini hadi sasa polisi hawakuingilia kati, na idadi ya waandamanaji inazidi kuongezeka.



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA