ZUMA KUTATUA MGOGORO WA LIBYA

Jacob Zuma
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewasili mjini Tripoli kwa kile kinachoonekana kuwa juhudi za mwisho za kujaribu kutafuta suluhu ya kidiplomasia ya mzozo unaoendelea.
Haifahamiki kama ziara hiyo ambayo ni ya pili kwa Bw Zuma, itaangazia kumshawishi Kanali Muammar Gaddafi kuondoka madarakani.
Waasi wanaopigana na majeshi ya Gaddafi tangu mwezi Februari wamekataa kufanya mazungumzo hadi pale atakapoondoka kwenye uongozi.
Wakati huo huo chama cha Bwana Zuma cha African National Congress kimeshutumu mashambulio ya majeshi ya Nato mjini Libya.
"Tunaungana na bara hili na watu wote wanaopenda amani duniani katika kushtumu mashambulio ya anga yanayoendelea Libya yakifanywa na vikosi vya magharibi," chama cha ANC kimesema katika taarifa siku moja kabla ya ziara ya Zuma.
Shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa zinaendelea dhidi ya Kanali Gaddafi, huku nchi zinazounda kundi la G8 zikitoa wito siku ya Ijumaa ya kumtaka aondoke na rais wa Urusi Dmitry Medvedev akisema siku ya Jumamosi kwamba hana tena haki ya kuwaongoza watu wa Libya.
Waasi wa Libya waliridhishwa na taarifa hiyo ya kundi la G8.
"Dunia nzima imekubaliana kwamba Kanali Gaddafi na utawala wake hawakupoteza tu uhalali wa kuongoza lakini pia heshima," alisema kiongozi wa waasi Mustafa Abdul Jalil katika taarifa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.