AFADHARI YA JELA

Bwana mmoja nchini Marekani anatarajiwa kwenda jela, baada ya kuingia benki na kutaka kuiba dola moja.
Gazeti la Telegraph limesema Bwana huyo James Richard Verone, aliingia benki na kumwambia mfanyakazi wa benki kuwa amekuja kuiba, na anataka dola moja tu.
Baada ya kutoa madai yake hayo, bwana huyo mwenye umri wa miaka hamsini na tisa, aliketi chini, na kusubiri polisi waje kumkamata.
Mwizi huyo, ambaye hana kazi na anakabiliwa na maradhi, amesema lifanya uhalifu huo, ili akamatwe na kufungwa, kwa kuwa anaamini jela ndio mahala pekee atapata huduma za afya.
"Mimi ni mtu wa busara" amesema bwana James "Nilitaka kuweka wazi kuwa nia yangu sio kuiba pesa, bali nahitaji kupelekwa hospitali".
Bwana huyo, ambaye hakutumia silaha yoyote wakati akifanya wizi hu, amesema ana imani kuwa huenda akapewa hukumu ya kifungo cha miaka mitatu jela, huku akipata huduma za hospitali.
Wizi huo ulitokea katika benki ya RBC, North Carolina

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA