Fundi Omar Mokiwa wa Idara ya Ujenzi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), akipanga vizuri mabati yenye bei nafuu yanayotengenezwa na mashine maalumu aina ya Ultimate Building Machine (UBM-120), katika banda la JWTZ kwenye maonesho hayo. Mashine hiyo hutengeneza mabati yanayoweza kuezekea paa na kujengea nyumba bada la ya matofali.
Ofisa Uhusiano wa ARPM, Hassan Abbas (katikati) akitoa ufafanuzi mbalimbali alipokuwa akiwawaeleza wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika maadhimisho hayo.
Ofisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Tagie Mwakawago akionesha picha za mawaziri waliowahi ongoza wizara hiyo tangu Uhuru hadi sasa, zilizopambwa kwenye banda la wizara hiyo katika maadhimisho hayo.
Comments