MAREKANI INAZUNGUMZA NA TALEBANI

Nchini Afghanistan Rais Karzai amethibitisha kuwa Marekani na mataifa mengine yanafanya mazungumzo ya awali na Taliban.


Watu walikisia kuwa Marekani ina mawasiliano na Taliban.
Lakini hilo ndio kwanza kuthibitishwa na kiongozi.
Rais Karzai amesema mazungumzo yanafanywa na Taliban, na kwamba jeshi la mataifa ya nje, hasa Marekani yenyewe, linafanya majadiliano.
Haijulikani nani wanaiwakilisha Marekani, na kama wanazungumza ana kwa ana na Taliban, au kuna mtu kati.
Kinachozungumzwa piya hakijulikani.
Msimamo rasmi wa Taliban ni kuwa majeshi ya kimataifa lazima kwanza yaondoke nchini kabla ya kujadili amani, na itazungumza na serikali ya Afghanistan tu.
Hayo hayalingani na yale aliyosema Rais Karzai.
Haifai kutaraji suluhu ya haraka kutokana na mawasiliano ya hivi sasa.
Utabiri wa pande zote, Nato, serikali ya Afghanistan na Taliban yenyewe, ni kuwa mapigano makali yataendelea kiangazi cha mwaka huu, na pengine miaka kadha ijayo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.