Hussein IssaMKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (Tazara ), Akashambatwa Lewanika amekamatwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam kwa kosa la kutohudhuria mahakamani aliposhitakiwa na wastaafu wa shirika hilo.Kukamatwa kwa mkurugenzi huyo kumefanya shughuli za kiutendaji kusimama kwa muda katika shirika hilo, baada ya maafisa wote kuhamia Kituo cha Polisi Chang’ombe.
Kwa mujibu wa habari ambazo Mwananchi ilizipata, mkurugenzi huyo alikamatwa jana asubuhi ofisini kwake huku wafanyakazi wastaafu wakishangilia kukamatwa kwake.
Chanzo cha habari kilisema kwamba mkurugenzi huyo hajawahi kutokea mahakamani wala kutuma mwakilishi tangu kuanza kwa kesi hiyo kati ya shirika hilo na wastaafu wanaodai fidia zao.Chanzo hicho cha habari kilisema kwamba kutokana na dharau hiyo ndiyo maana Jeshi la Polisi lilipomtia nguvuni kiongozi huyo.
Kamanda wa Jeshi Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime alisema kwamba yeye hana taarifa ya kukamatwa kwa mkurugenzi huyo kwa sababu alikuwa katika mkutano tangu asubuhi.“Kwa kweli sijui lolote, mimi tangu asubuhi nilikuwa katika mkutano na makamanda wenzangu,”alisema Misime.
Kwa mujibu wa habari ambazo Mwananchi ilizipata, mkurugenzi huyo alikamatwa jana asubuhi ofisini kwake huku wafanyakazi wastaafu wakishangilia kukamatwa kwake.
Chanzo cha habari kilisema kwamba mkurugenzi huyo hajawahi kutokea mahakamani wala kutuma mwakilishi tangu kuanza kwa kesi hiyo kati ya shirika hilo na wastaafu wanaodai fidia zao.Chanzo hicho cha habari kilisema kwamba kutokana na dharau hiyo ndiyo maana Jeshi la Polisi lilipomtia nguvuni kiongozi huyo.
Kamanda wa Jeshi Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime alisema kwamba yeye hana taarifa ya kukamatwa kwa mkurugenzi huyo kwa sababu alikuwa katika mkutano tangu asubuhi.“Kwa kweli sijui lolote, mimi tangu asubuhi nilikuwa katika mkutano na makamanda wenzangu,”alisema Misime.
Comments