NGOZI YA CHURA INATIBU SARATANI

Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Belfast wamejishindia tuzo kwa kazi waliyoifanya kuhusiana na ngozi ya chura ambayo wamegundua inaweza kutibu zaidi ya maradhi makuu 70.
Watafiti hao walipokea tuzo yao kwenye sherehe iliyoandaliwa na Tuzo ya ubunifu kutoka taasisi ijulikanayo kama Medical Futures Innovation mjini London.
Wataalamu hao wakiongozwa na Profesa Chris Shaw wa taasisi ya Famacia ya Queens, wamegundua proteni mbili ambazo zinaweza kurekebisha kukuwa kwa mishipa ya damu.
Waligundua kuwa proteni kutoka aina ya chura ajulikanaye kwa jina la kitaalamu 'waxy monkey frog' hubana kukuwa kwa mishipa inayosambaza damu mwilini na inaweza kutumiwa kuua uvimbe unaotokana na saratani.
Profesa Shaw alisema kuwa mara nyingi uvimbe huo huweza kuchochewa kufikia kiwango fulani kabla ya kuhitaji damu zaidi ili kupevuka kuwa kivimbe ambacho husaidia kupitisha hewa ya oksijeni na lishe.
Kwa hiyo akaongezea kusema '' Ili kusitisha kukuwa kwa mishipa hii isikuwe hadi kuvimba kutafanya saratani isienee na hatimaye kuiondoa mwilini kabisa.
Hili lina uwezekano mkubwa wa kuifanya saratani yawe maradhi yasiyo uwa ila ya kuishi nayo.
Kundi hilo liligundua pia kuwa aina ya chura mkubwa ajulikanaye kama ''firebellied toad'' huzalisha proteni inayoweza kuchagiza mishipa kukuwa na inaweza kusaidia katika kutibu majeraha ya mgonjwa yapone kwa haraka zaidi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI