PWEZA WANNE KUSHINDANA UJERUMANI

Pweza wanane nchini Ujerumani watashindanishwa kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la soka kwa wanawake itakayoanza hivi karibuni.
Pweza hao watashindanishwa kutafuta mrithi wa pweza Paul, aliyepata umaarufu wa kutabiri matokeo ya mechi za soka za Kombe la Dunia mwaka jana Afrika Kusini.
"Kwa sasa tunawafanyia mazoezi na mafunzo tukiwa na matumaini ya kupata japo mmoja atakayeweza kutabiri" amesema Britta Analauf, msemaji wa idara inayoandaa michuano ya Kombe la Dunia.
Kila siku kuanzia saa tano kamili asubuhi pweza hao wanane, waliopo katika miji tofauti watakuwa wakipewa mitihani ya kutabiri mambo mbalimbali.
Pweza hao wanatoka miji ya Hanover, Koenigswinter, Konstanz, Minich, Speyer, Timmendorfer Stand, na mji aliotoka Paul, Oberhausen.
Utabiri huo wa mazoezi haujatajwa rasmi, lakini gazeti la Metro limesema itakuwa ikilingana kidogo na kile alichokuwa akifanya Pweza paul mwaka jana, pale alipojizolea sifa za kubashiri sawasawa matokeo ya mechi zote saba za Ujerumani.
Pweza Paul alifariki dunia akiwa na umri wa karibu miaka mitatu, mwezi Oktoba mwaka jana.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI