WAASI DRC CONGO WABAKA WANAWAKE

Wanawake wakiandamana Congo kupinga ubakaji


Wafanyakazi wanaotoa misaada wanafanya uchunguzi wa ripoti iliyosema takriban wanawake 60 wamebakwa karibu na mji wa Fizi uliopo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ubakaji huo wa wanawake wengi unadaiwa kufanywa na kundi la waliokuwa waasi ambao hivi karibuni waliasi jeshi la serikali, ambao waliungana chini ya makubaliano ya amani.
Majeshi kutoka kundi hilo hilo hivi karibuni walishtakiwa kwa kubaka takriban wanawake 50 huko Fizi siku ya mwaka mpya.


Ujumbe wa umoja wa mataifa mwaka jana uliipa jina nchi hiyo ya DRC "mji mkuu wa ubakaji duniani".
Miaka 16 ya ghasia mashariki mwa Congo imejulikana kwa udhalilishaji wa wanawake na wasichana.
Zaidi ya wanawake 300, wanaume na watoto walibakwa na muungano wa kundi la waasi kwenye mji wa Luvungi na vijiji jirani katika jimbo la Kivu Kaskazini ambalo halikuwa mbali sana na kituo cha umoja wa mataifa mwezi Agosti 2010.
Tukio la hivi karibuni lilitokea vijijini karibu na Fizi, Kivu kaskazini kati ya Juni 10 na 12 lakini ndio kwanza imeripotiwa.
Jean-Marie Ngoma, mwanachama wa bunge la jimbo hilo, ameiambia redio inayofadhiliwa na umoja wa mataifa ya Okapi kuwa zaidi ya wanawake 60 walibakwa kwenye kijiji cha Nyakiele peke yake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*