WIKI YA UTUMISHI WA UMMA YA UN,AFRIKA YAENDELEA

Ofisa Uhusiano wa Pensheni ya Watumishi wa Serikali (PSPF), Fatma Elhady (kushoto), akitoa maelezo kwa watumishi wa umma, jinsi ya kukamilisha ujazaji fomu za pensheni katika maadhimisho hayo yanayofikia kilele kesho kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wakiangalia mashine ya kukoboa nafaka iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga la Jeshi la Wananchi Tanzania (JWZT). Mashine hiyo inayouzwa sh. 1,200,000 inaoneshwa kwenye maadhimisho hayo.




Ofisa Kumbukumbu wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ismail Said (kushoto), akitoa maelezo kwa wananchi, jinsi wanavyotambua vitu mbalimbali kwa kutumia vinasaba (DNA), katika maadhimisho hayo.





Mkaguzi Mwandamizi wa Vyakula wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Moses Mbambe akionesha mvinyo ambao ni sehemu ya vyakula na dawa feki zinazooneshwa kwenye banda la TFDA, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ya Umoja wa Mataifa na Afrika yanyofikia kilele leo kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA)






Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wakipata maelezo ya majukumu ya Tume ya Utumishi wa Umma, katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ya Umoja wa Mataifa na Afrika, katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.









Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI