Aliyekuwa kiongozi Guatemala kushtakiwa

Aliyekuwa kiongozi wa kijeshi nchini Guatemala, Efrain Rios Montt, atashtakiwa kwa kuhusika katika mauaji ya halaiki na uhalifu dhidi ya binadamu.

Jaji katika mahakama maalum iliyokuwa ikisikiliza kesi dhidi yake amesema kuwa kuna ushahidi wa kutosha wa kumshtaki na amemhukumu kifungo cha kutotoka nyumbani hadi kesi hiyo iaamuliwe.

Kiongozi huyo wa zamani alifikishwa katika mahakama kuu kusikiza tuhuma kadhaa dhidi yake. Mahakamani familia za waathirika wa mauaji hayo waliofika walimzomea kwa maneno makali.

Anatuhumiwa kutekeleza mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya binadamu, ikiwemo mauaji ya watu zaidi ya 1,770, ubakaji wa wanawake 1,500 na kuwatimua watu 29,000 kutoka makwao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA