ANC yamazila sherehe za kutimiza karne

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amehutubia maelfu ya wafuasi wa ANC, katika sherehe zinazomalizika leo za kuadhimisha miaka 100 tangu chama hicho kuundwa - chama kikongwe kabisa cha ukombozi barani Afrika.
Mauaji ya Sharpeville, Afrika Kusini mwaka wa 1960
Bwana Zuma alisema leo ni siku ya furaha kwa watu wa Afrika Kusini, ambao waliangamiza ukoloni na ubaguzi wa rangi, kwa kusaidiwa na Afrika na ulimwengu.

Bwana Nelson Mandela hakuweza kuhudhuria kwa sababu ni dhaifu.

ANC hivi karibuni imekumbwa na kashfa za rushwa na mizozo ndani ya chama lakini bado kina wafuasi wengi

Kati ya wageni waliohudhuria sherehe hizo ni Kasisi Jesse Jackson, mwanaharakati maarufu wa Marekani wa kutetea haki za weusi.

Alisema: "Baada ya karne moja - kutoka madhalilisho, kachomoza Nelson Mandela, Thabo Mbeki, Jacob Zuma, na Barack Obama.

Ni karne ya mifano ya kuvuka vizingiti vikubwa.

Na khofu waliyokuwa nayo wazungu - kwamba weusi watalipiza kisasi - hayakutokea hayo".

.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA