bo Hoyce Temu Alamba Nondozz chuo cha Diplomasia
Afisa
Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania
1999 na Mwandishi wa kitabu NAYAKUMBUKA YOTE Hoyce Temu akisubiri
kutunukiwa Stashahada ya Uzamili katika Menejimenti ya Mahusiano ya
Kimataifa (Post Graduate Diploma in Management of Foreign Relations) katika Mahafali ya Kumi na Sita ya Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Benard Membe
akimtunukia Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa ambaye amewahi kuwa
Miss Tanzania 1999 na Mwandishi wa kitabu NAYAKUMBUKA YOTE Hoyce Temu
Stashahada ya Uzamili katika Menejimenti ya Mahusiano ya Kimataifa
(Post Graduate Diploma in Management of Foreign Relations) katika
Mahafali ya Kumi na Sita ya Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam.
Hoyce
Temu katika picha ya pamoja na familia yake. Kutoka kushoto ni Mrs.
Shose Minja mama yake mdogo, Pendo Matee Makwaiya, Rafiki yake Emelda
pamoja na dada yake Edith Max.
Hoyce Temu katika picha ya pamoja na rafiki yake Mrs Mareale
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Benard Membe katika Picha ya Pamoja na wahitimu Stashahada
ya Uzamili katika Menejimenti ya Mahusiano ya Kimataifa (Post Graduate
Diploma in Management of Foreign Relations). Wa tatu kutoka kushoto
waliosimama ni Hoyce Temu. Blogu ya kamanda wa Matukio inakubongeza kwa juhudi zako za kusaka zaidi elimu.
Comments