Boko Haram wauwawa Nigeria

Jeshi la Nigeria linasema limewapiga risasi na kuwauwa wafuasi 11 wa kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu, Boko Haram, kaskazini-mashariki mwa nchi.
Watu waliouliwa na Boko Haram

Msemaji wa jeshi alieleza kwamba wapiganaji hao waliuwawa wakati wa mapambano katika mji wa Maiduguri, ambako kundi hilo lilianzishwa mwongo uliopita.

Juma lilopita watu kama 185 waliuwawa katika mji mwengine wa kaskazini, Kano, kwenye mashambulio kadha ya mabomu.

Boko Haram ilisema ilifanya mashambulio hayo, na imeonya kuwa itaendelea na ugaidi hadi mfumo wa sharia unafuatwa Nigeria nzima.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA