Bomu lauwa watu 50 Iraq


Wakuu wa Iraq wanasema mtu aliyejitolea mhanga ameripua bomu na kuuwa watu kama 50, katika shambulio dhidi ya mahujaji wa Kishia katika mji wa Basra, kusini mwa nchi.
Shambulio dhidi ya mahujaji wa Kishia, Iraq

Inaarifiwa kuwa watu 90 wengine wamejeruhiwa.

Polisi walieleza kuwa mahujaji hao walikuwa wanaelekea msikiti mkubwa wa Washia nje ya Basra, mwisho wa ile wanayoita Arbain, moja kati ya vipindi vinavyoadhimishwa na Washia.

Askari wa usalama 7 ni kati ya watu waliokufa.

Shambulio hilo linakuja wakati mvutano wa kisiasa unazidi baina ya Washia, walio wengi Iraq, na Wasunii.

Mwezi uliopita, serikali yenye Washia wengi, ilitoa amri ya kumkamata makamo wa rais aliye wa madhehebu ya Sunni, Tariq al-Hashemi, kwa mashtaka ya ugaidi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA