Katibu
wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
akizungumza na waandishi wa habari leo katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu
ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, kuhusu maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM
ambayo yataanza mwanzoni mwa mwezi Februari na kufikia kilele chake
Februari 5, 2012.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema maadhimisho ya kuzaliwa kwake ya
mwaka huu pamoja na mambo mengine kitayatumia kupiga vita wagombea wote
wanaotoa na kupokea rushwa wakati wake mkuu.
Pia kitatumia maadhimisho hayo kuhamasisha wananchama wake waadilifu na
waaminifu kujitokeza kugombea katika uchaguzi huo utakaofanyika mwaka
huu, kuanzia ngazi za mashina hadi taifa.
Hayo yalisemwa leo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi
na Uenezi, Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari,
kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam.
Nape alisema, Chama kitatumia fursa hiyo pia kuwaelimisha wanachama wake
na wananchi kwa jumla kuhusu mabadiliko ya Katiba ya nchi
yanayokusudiwa kufanyika, ikiwa ni pamoja na msimamo wa kuilinda nchi,
amani, na kupatikana kwa Katiba bora itakayokuwa na manufaa kwa watu
wote.
Alisema, maadhimisho hayo yataanza Februari mosi na kufikia kilele chake
Februari 5, 2012 yakiambatana na shughuli mbalimbali yakiwemo matembezi
ya mshikamano yatakayofanyika kila mkoa wakati Mwenyekiti wa CCM, Rais
Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi katika kilele cha matembezi hayo
kitakachofanyika Mwanza.
Nape alisema .
"Maadhimisho haya ni kumbukumbu muhimu kwa Chama Cha Mapinduzi kufikisha
miaka 35 ya uhai wake yangu vyama vya TANU na ASP vilipovunjwa na
kuundwa chama kipya cha CCM chenye nguvu, Februari 5, 1977",lisema Nape
na kuongeza.
"Sherehe hizo huadhimishwa kwa Chama na Jumuia zake kufanya shughuli
mbalimbali za kisiasa na kijamii. Aidha, Kitaifa Chama huteua mkoa
mwenyeji wa sherehe hizi ambazo huambatana na matembezi ya mshikamano".
Alisema kwa kuwa mwaka huu ni wa Uchaguzi Mkuu wa Chama kimependekeza
kaulimbiu mahsusi itakayotumika katika sherehe hizo kuwa ni "CCM Imara
na Madhubuti inaanza na mimi; naimarisha Chama Changu kwa kuchagua
viongozi bora na waadilifu".
Nape alisema uzinduzi wa sherehe hizo utafanyika kila mkoa Januari 30,
mwaka huu na kufuatiwa na wiki ya shughuli za Jumuia, ambazo kila Jumuia
itapanga ratiba ya mikutano ya ndani na shughuli za kijamii kama
kupanda miti.
CCM imewataka wajumbe wa Kamati ya Siasa na Halmashauri Kuu ya mikoa
kutumia wiki hiyo kufanya ziara katika matawi kuimarisha uhai wa Chama.
MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, Hawa wanapatikana kusini mwa Tanzania ni kab
Comments