CCM YAMTEUA RAZA KUGOMBEA UWAKILISHI JIMBO LA UZINI
Mohammed Raza |
Kamati Kuu ya CCM imemteua mwanachama wake, Mohammed Raza kuwa mgombea wa Uwakilishi jimbo la Uzini.
Katibu
wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
alisema kwamba kikao hicho kilichofanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM,
Rais Jakaya Kikwete kimempitisha Raza baada ya kuridhika na sifa zake.
Nape
alisema, Kamati Kuu pia imemteua Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar),
Dk. Aman Karume kufungua kampeni za CCM za kuwania jimbo hilo ambazo
zitafanyika Januari 28, mwaka huu katika Uwanja wa mpira wa Ghana.
Alisema
wakati kampeni zitafunguliwa na Dk. Karume, ufungaji kampeni hizo
utafanywa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kwenye Uwanja wa mpira wa
Tunduni.
Uchaguzi
mdogo wa uwakilishi jimbo la Uzini unafanyika kufuatia kufariki dunia
aliyekuwa mwakilishi wake kwa tiketi ya CCM, Mussa Hamis Silima
aliyefariki kwa ajali ya gari, Septemba 23, mwaka jana.
Kuhusu
minong’ono kwamba Raza ana utata katika uraia wake, Nape alisema Kamati
Kuu imelitaza jambo hilo kwa makini lakini haikuweza kulipa uzito wa
kumyima Raza nafasi ya kugombea kwa kuwa hakuna ushahidi wowote
uliowasilishwa kuthibitisha hilo.
“Bado
tunao muda wa kutosha, kama yupo mwenye ushahidi wa kutosha kuhusu hili
anaweza kuleta ushahidi, ukiwa na uzito hatutaupuuza”, alisema Nape.
Comments