GHANA YAINGIA ROBO FAINALI AFRICA

Ghana inaelekea kufuzu kwa robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya Jumamosi kuishinda Mali magoli 2-0.

Andre Dede Ayew

Ayew aliyepokea tuzo la BBC la mchezaji bora hivi majuzi alionyesha ustadi kwa kufunga bao la pili la Black Stars

Asamoah Gyan ndiye aliyefunga bao la kwanza la Black Stars.

Andre 'Dede' Ayew kisha aliwachanganya walinzi wa Mali na kupitia nafasi iliyojitokeza, aliandikisha bao la pili la Ghana.

Awali Cheick Diabate mara mbili ilikuwa nusra aifungie Mali magoli, lakini kweli bahati haikuwa yake, kwani mipira yote iligonga goli, lakini kamwe mpira ulikataa kugusa nyavu katika mechi hiyo iliyochezewa mjini Franceville.

Ghana inaongoza kundi D kwa pointi sita, lakini kimahesabu, mataifa ya Guinea na Mali bado yana nafasi ya kufuzu kuingia robo fainali.

Guinea kwa hakika ilithibitisha uwezo wake katika mashindano hayo kwa kuiangamiza bila huruma Botswana, magoli 6-1, katika mechi ambayo pia ilichezewa mjini Franceville.

Guinea inatazamia wingi huo wa mabao huenda ikawa jambo zuri, na inasubiri kwa hamu kusikia matokeo ya mechi kati ya Mali na Botswana Jumatano ijayo mambo yatakuwa vipi, na wakati ambao wao watacheza na Ghana.

Lakini kumbuka Jumapili kuna mechi za kuvutia pia, wakati wenyeji wenzao Guinea wakipumzika, Equatorial Guinea watakuwa na kibarua cha kucheza na Zambia mjini Malabo, huku Libya nayo ikicheza na Senegal mjini Bata.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA