HALMASHAURI ZOTE KUANZA KUTUMIA MFUMO MMOJA WA KIHASIBU HIVI KARIBUNI.

Halmashuri zote hapa nchini zinatarajia kutumia mfumo mmoja wa kihasibu ambapo kupitia mfumo huo taarifa za kihasibu pamoja na takwimu mbalimbali za idara hiyo zitaweza kuonekana kwa urahisi zaidi tofauti na mfumo uliokuwepo hapo zamani.
hayo yameelezwa leo na Bw Jeremiah Mtawa ambaye ni Mwenzeshaji wa kitaifa wa mfumo huo kutoka Tamisemi wakati akizungumza na waandshi wa habari mara baada ya kufungua mkutano kwa wadau mbalimbali wa halmashauri mkoani hapa.
Bw Jeremiah alisena kuwa kwa sasa mfumo huo utakuwa na faida kubwa sana hata kwa upande wa wahasibu ndani ya halmashauri kwa kuwa mfumo huo ni raisi zaidi kiutendaji kuliko ule wa awali.
alibanisha kuwa pia mfumo huo ambao unajulikana kwa jina la mfumo wa uhasibu usimamizi na udhibiti wa fedha za umma utaweza kuraisisha shuguli mbalimbali za kihasibu.
"hapo awali mfumo wa kihasibu uliokuwepo ulikuwa una mambo mengi sana lalkini kwa sasa mfumo huu ambao unatumia teknolojia mbalimbali utaweza kusaidia sana kazi hii kwa msingi wa hali ya juu sana"aliongeza Bw Jeremia.
pia alisema kuwa nao watumiaji wa mfumo huo wanatakiwa kuwa makini sana na kuhakikisha kuwa wanafuta taratibu na sheria mbalimbali za mfumo huo ili kufikia malengo mbalimbali ambayo yamekusudiwa.
alianisha kuwa endapo kama watafuata sheria na kanuni mbalimbali za mfumo huo basi halmashauri mbalimbali hapa nchini zitaweza kuepukana na madhara mbalimbali huku kwa upande wa Serikali nako malengo yake yakiweza kutimia . (kwa hisani ya Fullshangwe blog)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA