JAMAA LAKATAA KUTOKA JELA

Bwana mmoja nchini Marekani ameshtakiwa baada ya kugoma kutoka jela. Gazeti la Arizona Daily Sun limesema bwana huyo alikamatwa wiki iliyopita kwa kosa la kuingia eneo lililopigwa marufuku, lakini alitakiwa kuachiliwa huru siku ya Jumatatu baada ya kutambua kosa lake.

Hata hivyo, bwana huyo aitwaye Martin Batieni Kombate, aligoma kutoka katika jela ya wilaya ya Coconino.

Maafisa wa polisi walipofika kumwambia kuwa yuko huyo na kumtaka atoke jela, bwana Martin alisema, hana mpango wowote wa kutoka kizuizini humo. Aidha polisi zaidi walipoitwa kutaka kufahamu kwa nini hataki kutoka jela, bwana huyo alisingizia kuwa hataondoka selo kwa sababu amepoteza pochi yake. Licha ya maafisa wa polisi kuendelea kumweleza kuwa sasa yuko huru, bwana Martin alikataa kata kata kutoka jela, hata baada ya kubembelezwa mara kadhaa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA