JAMAA LAKATAA KUTOKA JELA

Bwana mmoja nchini Marekani ameshtakiwa baada ya kugoma kutoka jela. Gazeti la Arizona Daily Sun limesema bwana huyo alikamatwa wiki iliyopita kwa kosa la kuingia eneo lililopigwa marufuku, lakini alitakiwa kuachiliwa huru siku ya Jumatatu baada ya kutambua kosa lake.

Hata hivyo, bwana huyo aitwaye Martin Batieni Kombate, aligoma kutoka katika jela ya wilaya ya Coconino.

Maafisa wa polisi walipofika kumwambia kuwa yuko huyo na kumtaka atoke jela, bwana Martin alisema, hana mpango wowote wa kutoka kizuizini humo. Aidha polisi zaidi walipoitwa kutaka kufahamu kwa nini hataki kutoka jela, bwana huyo alisingizia kuwa hataondoka selo kwa sababu amepoteza pochi yake. Licha ya maafisa wa polisi kuendelea kumweleza kuwa sasa yuko huru, bwana Martin alikataa kata kata kutoka jela, hata baada ya kubembelezwa mara kadhaa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.