Kagame ataka Wenger aondoke

Rais wa Rwanda Paul Kagame amemtaka kocha wa klabu ya soka ya Arsenal, Arsene Wenger kuachia ngazi.

Kagame ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo yenye makao yake kaskazini mwa jiji la London. Rais Kagame amempiga kigongo hicho Mfaransa Wenger baada ya Arsenal kuchapwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Manchester United wiki iliyopita.

Huo ulikuwa mchezo wa tatu kwa Arsenal kupoteza mfululizo. "Naipenda sana Arsenal, lakini kusema kweli Wenger anahitaji kufundisha timu nyingine, na Arsenal inahitaji kocha mwingine" amekaririwa Kagame kupitia mtandao wa Twitter. Gazeti la Sun la hapa Uingereza limesema Rais huyo amesema wakati sasa umewadia kwa klabu hiyo kufanya mabadiliko.

Wenger amekuwa kocha wa Arsenal tangu mwaka 1996, na mara ya miwsho kushinda kombe lolote ilikuwa mwaka 2005.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*