Rais wa Rwanda Paul Kagame amemtaka kocha wa klabu ya soka ya Arsenal, Arsene Wenger kuachia ngazi.
Kagame ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo yenye makao yake kaskazini mwa jiji la London. Rais Kagame amempiga kigongo hicho Mfaransa Wenger baada ya Arsenal kuchapwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Manchester United wiki iliyopita.
Huo ulikuwa mchezo wa tatu kwa Arsenal kupoteza mfululizo. "Naipenda sana Arsenal, lakini kusema kweli Wenger anahitaji kufundisha timu nyingine, na Arsenal inahitaji kocha mwingine" amekaririwa Kagame kupitia mtandao wa Twitter. Gazeti la Sun la hapa Uingereza limesema Rais huyo amesema wakati sasa umewadia kwa klabu hiyo kufanya mabadiliko.
Wenger amekuwa kocha wa Arsenal tangu mwaka 1996, na mara ya miwsho kushinda kombe lolote ilikuwa mwaka 2005.
Comments