Kenya yasema al-Shabaab yasambaratika

Jeshi la Kenya linasema kuwa kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, al-Shabaab, kinasambaratika, huku shambulio la Kenya nchini humo linamezidi kuwa na kasi.
Ndege ya jeshi la Kenya

Msemaji wa jeshi la Kenya, Kanali Cyrus Oguna, aliwaambia waandishi wa habari mjini Nairobi, kwamba mgawanyiko kati ya viongozi wa al-Shabaab unamaanisha kuwa mwisho wa kikundi hicho hauko mbali.

Alisema mashambulio yaliyofanywa na ndege za Kenya hapo jana yaliuwa wapiganaji wa al-Shabaab kama 60, na kwamba wapiganaji 20 wamejiunga na upande wa jeshi la Kenya, katika muda wa majuma mawili.

Lakini mwandishi wa BBC Afrika Mashariki, anasema ni shida sana kuthibitisha taarifa hizo.

Al-Shabaab inasema itawashinda Wakenya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA