ZUKU TV WAZINDUA RASMI HUDUMA ZAO NCHINI
Mkurugenzi
wa TCRA,Profesa John Mkoma akibonyeza
kitufe ikiwa ni ishara ya kuzindua Televisheni ya Zuku Africa kupitia kampuni ya
Wananchi Satelite Tanzania inayotoa matangazo yake kwa kutumia ving'amuzi nchini
Tanzania , Hafla ya uzinduzi iliyofanyika kwenye hoteli ya Golden Tulip jijini
Dar es salaam jana jioni ikihudhuriwa na wadaum mbalimbali na wageni
waalikwa. Katika picha kulia ni Richard Bell Afisa Mtendaji
Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group na kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya
Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki wakishuhudia tukio hilo.
Mkurugenzi wa TCRA,Profesa
John Mkoma mbele ya wageni waalikwa mbalimbali kabla ya kuzindua kampuni ya
Wananchi Satelite jana katika hafla iliyofanyika jana kwenye hoteli ya Golden
Tulip kulia ni Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya
Wananchi Group na kulia ni Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group Bw. Ali
Mufuruki
Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi
Group Bw. Ali Mufuruki akizungumza katika uzinduzi huo na kumkaribisha
Mkurugenzi wa TCRA Profesa John Mkoma. Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa
makampuni ya Wananchi Group akimkaribisha Mwenyekitiwa Makampuni ya
Wananchi Group Ali Mufuruki.
Bendi ya Tanzanite ikiongozwa na mwanamzuiki nguli
John Mhina ilitoa burudani ya kutosha katika uzinduzi huo jana.
Waimbaji wa muziki wa injili pamoja na waigizaji wa
filamu hawakukosa uzinduzi huop kutoka kulia ni Mwigizaji Natasha, Monalisa ,
Mwimbaji Alice na mumewe ambaye pia ni mwimbaji Bw. Robert David wakipozi kwa
picha.
Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa
makampuni ya Wananchi Group katikati na Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi
Group Bw. Ali Mufuruki kulia wakimsikiliza Meneja mkuu wa Wananchi
Satelite Bw Mohamed Jeneby akiwaelezea jambo.
Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa
makampuni ya Wananchi Group kulia i na Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group
Bw. Ali Mufuruki wakijadili jambo katika uzinduzi huo.
Mamaa Shamimu Mwasha a.k.a. ZEZE wa http://8020fashions.blogspot.com/akitafuta
taswira katika uzinduzi huo, kuminya jicho ni lazima kama unataka taswira
iliyotukuka.
Comments