Maiti mbili zapatikana melini Utaliana

Mlinzi wa pwani katika kisiwa cha Giglio, Utaliana, anasema maiti za wanaume wawili wazee zimekutikana katika upande uliozama wa meli ya abiria iliyokwenda mrama, Costa Concordia.
Idadi ya watu waliokufa imefikia watano, tangu meli hiyo kufikwa na ajali Ijumaa usiku.
Watu wengine kadha wametoweka.
Nahodha wa meli anahojiwa, kujaribu kujua chanzo cha ajali.
Aliiambia televisheni ya Utaliana kwamba, kufuatana na ramani zake, meli ilikuwa mbali vya kutosha na ufukwe, na isingetarajiwa kugonga mwamba.
Hapo awali, afisa mmoja wa meli hiyo aliyejeruhiwa, aliokolewa na kupelekwa hospitali.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*