Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kalenga, Iringa, Steven Galinoma amefariki Dunia leo alipokuwa akikimbizwa hospitali , kuokea Kalenga alikokuwa akiishi.
Marehemu Steven Galinoma amefariki leo tarehe 26 Januari, 2012 saa 4.00 asubuhi akiwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Misheni ya Ipamba iliyopo Iringa Vijijini kwa matibabu kutokana na ugonjwa wa saratani akitokea kijijini kwake Kalenga.
Enzi za uhai wake, Marehemu Steven Galinoma pia aliwahi kufanya kazi Serikalini kwa muda mrefu na kushika nyadhfa mbalimbali hadi kufikia wadhfa wa Katibu Mkuu katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Marehemu Steven Galinoma amefariki leo tarehe 26 Januari, 2012 saa 4.00 asubuhi akiwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Misheni ya Ipamba iliyopo Iringa Vijijini kwa matibabu kutokana na ugonjwa wa saratani akitokea kijijini kwake Kalenga.
Enzi za uhai wake, Marehemu Steven Galinoma pia aliwahi kufanya kazi Serikalini kwa muda mrefu na kushika nyadhfa mbalimbali hadi kufikia wadhfa wa Katibu Mkuu katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Comments