MKUU WA MKOA RUKWA ATEMBELEA MKANDARASI AASLEFF BAM INTERNATIONAL ANAYEJENGA BARABARA YA LAELA-SUMBAWANGA , ATANGAZA VITA NA WEZI WA MAFUTA NA VIFAA

Eneo hili ambalo lipo nje kidogo na kambi ya Mkandarasi huyo linatumika kwa ajili ya uchimbaji, upasuaji, na hatimaye utengenezaji wa kokoto kwa ajili ya kuweka lami katika barabara anayojenga mkandarasi huyo. Aasleff Bam International inajenga barabara ya Laela- Sumbawanga (95.31 Km) kwa kiwango cha lami. Barabara ya Tunduma- Laela- Sumbawanga kufikia kiwango cha lami imegawanywa sehem kuu tatu ikiwemo Tunduma- Ikana (63.7 Km), Ikana- Laela (64.2 Km ) na Laela- Sumbawanga (95.31 Km ). Kwa habari na picha zaidi Tembelea hapa:http:http//:www.rukwareview.blogspot.com/
Barabara hii inaendelea kujengwa na mpaka sasa kipande hiki cha Laela- Sumbawanga kinachojengwa na Aasleff Bam Internatinal kimeshakamilika kwa takriban aslimia 25% na tayari kuna kilomita 10 za majaribio zimeshawekwa lami. Kandarasi huyo pamoja na wengine waliopo Mkoani Rukwa wanatakiwa kukabidhi barabara zote mwanzoni mwa mwaka 2013.
Kutoka muda uliopangwa Mkandarasi huyu ameomba kuongezewa muda wa miezi minne kutokana na sababu kuu tatu, moja ikiwa ni kuchelewa kufika kwa vifaa vya ujenzi walivyoagiza kutoka nje ya nchi, kucheleweshwa vifaa hivyo bandarini kwani vilichukua muda wa miezi minne, na ukubwa wa kazi iliyopo kuwa chini ya makisio yao hivyo kuchukua muda mwingi wa majadiliano namna ya kukamilisha kazi kubwa kwa gharama za makisio madogo.
Injinia Manyanya akishikana mikono na mmoja wa makandarasi wa Aasleff Bam mara baada ya kupewa maelezo juu ya mashine inayoonekana nyuma yao ya kuchanganya udongo na cement. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Kanali John Antonyo Mzurikwao na Kushoto ni Meneja wa Tanroads Mkoa wa Rukwa Kabaka Florian Mwombeki.
Msafara wa Mkuu wa Mkoa ukipokea maelezo kutoka kwa Mkandarasi wa Aasleff Bam kuhusu ujenzi wa barabara unaoendelea.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na wakandarasi wa Kampuni ya Aasleff Bam International ya Uholanzi inayojenga barabara ya Laela - Sumbawanga kwa kiwango cha lami katika Mkoa huo. Mkuu huyo wa Mkoa alilazimika kufanya ziara kujionea hali ya ujenzi inavyoendelea pamoja na kuzungumza na wafanyakazi wa Kampuni hiyo. Kulia ni Mashine aina ya mixer inayochanganya udongo na cement na kunyoosha barabara kabla ya kokoto ngumu na lami kuwekwa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wazawa wa kampuni ya Aasleff Bam International ya Uholanzi inayojenga barabara ya Laela - Sumbawanga kwa kiwango cha lami. Aliomba kuzungumza na wafanyakazi hao kutokana na kulaumiwa kuiibia kampuni hiyo vifaa ikiwepo mafuta ya diesel zaidi ya lita 30,000, tani 40 za simenti , na nondo zaidi ya tani 300.
Mkuu huyo wa Mkoa aliwaasa wafanyakazi hao kuwa na moyo wa kizalendo kwa kuona kuwa kazi anayofanya kandarasi huyo italeta manufaa kwao. Alitangaza vita na yeyote yule atakayethibitika kuhusika na wizi katika kampuni hiyo pamoja na kampuni zingine zinazofanya kazi hiyo ya ujenzi Mkoani Rukwa. Alisema kuwa ni aibu kuona wizi wa namna hiyo kwani kazi anayofanya kandarasi huyo ni kwa manufaa ya watanzania wenyewe.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA