Mtoto aiba gari la baba

Mtoto mmoja wa miaka kumi nchini Ufaransa anashikiliwa na polisi, baada ya kuchukua gari la baba yake na kujaribu kwenda nalo shuleni kwao, baada ya kuachwa na basi la shule.

Kijana huyo, ambaye alimpakiza mwenzake mwenue umri wa miaka tisa, na ambaye pia alikuwa ameachwa na basi la shule, walifanikiwa kuendesha gari hilo kwa umbali wa kilomita mbili, kabla ya kugonga ukingo wa barabara, wameripoti polisi wa mji wa Valence.

"Nilikuwa nimevaa mkanda" amejitetea kijana huyo baada ya polisi kuwasili eneo la tukio. Vijana hao hawakuumia. Polisi wamesema kijana huyo huenda akashtakiwa kwa kosa la kuendesha gari bila ya kuwa na leseni, na kuharibu barabara ya umma.

Lakini waendesha mashtaka watafanya uamuzi kuona kama wafungue kesi au la.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA