MWANRI AWASHAMBULIA WANAOPINGA UTENDAJI WA SERIKALI YA JK
Na Francis Godwin,Mufindi
NAIBU
waziri ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa
(TAMISEMI) Agrrey Mwanri amewataka wananchi kuwapuuza viongozi wa vyama
vya upinzani ambao wamekuwa wakihamasisha wananchi kuichukia serikali ya
Rais Jakaya Kikwete bila kuwahamasisha vijana kufanya kazi kwa
kujituma.
Alisema
kuwa kila kukicha kumekuwa na migomo na maandamano ya kudai haki zao
bila viongozi hao kuwahamasisha vijana hao kufanya kazi badala ya
kuendelea kukaa vijiweni na kufanya maandamano ya kudai maisha bora bila
kufanya kazi.
Akiwaahutubia
wakazi wa Lugorofu Mgololo wilaya ya Mufindi Jana Mwanri alisema kuwa
vijana wasikubali kutumikishwa na vyama hivyo vya siasa ambavyo sera
zake ni kuikosoa serikali iwe kwa jema ama bay a na mud a wote wao ni
kufanya maandamano ya kuipinga serikali.
Hivyo aliwataka vijana kufanya kazi kwa nguvu zote na Kuacha kuendelea kushinda vijiweni na kulalamikia ugumu wa maisha.
Katika
hatua nyingine Mwanri amepiga marufuku Halmashauri kuendelea kutoa kazi
kwa wakandarasi ambao wamekuwa wakija na vibarua wao katika kutekeleza
miradi ya ujenzi katika Halmashauri husika na kuwa ni vema wakandarasi
hao kuwatumia wananchi na vijana wa eneo husika na sio nje ya mradi .
Naibu
waziri huyo Mwanri kwa Mara ya kwanza amepongeza kazi nzuri ya ujenzi
wa mfereji wa umwagiliaji Mgololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa mradi
uliojengwa kwa kiasi cha zaidi ya shillingi bilioni moja na kuagiza
maofisi ugani katika Halmashauri hiyo na Halmashauri nyingine za mkoa wa
Iringa kutoka maofisini na Kwenda mashambani kusaidia
Katika
ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya
ya Mufindi jana ,Mwanri alisema kuwa Amevutiwa na kazi nzuri ya
usimamizi wa fedha za miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo ya
Mufindi na kuwa baadhi ya Halmashauri za mkoa wa Iringa wakurugenzi wake
na wahandisi wa miradi ya ujenzi na maji Kama wilaya ya Ludewa
wameshindwa Kabisa kuwajibika katika kusimamia fedha za serikali na
wahisani katika miradi hiyo.
Hivyo
alisema kuwa Wizara yake haitawafumbia macho watendaji wabovu
wanaoshindwa kusimamia miradi hiyo ya maendeleo na kuwa katika ziara
yake Halmashauri ya wilaya ya Mufindi imeonyesha kuwa ni Halmashauri ya
mfano kwa kuwa na mradi mzuri wa umwagiliaji ambao bado kukamilika ila
ni mradi wenye Sita zote za kuitwa mradi wa umwagiliaji.
Mwanri
alisema kuwa pamoja na kuwa mradi huo bado kukamilika ila amelazimika
kuruhusu uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi kupitia mkurugenzi
wake Shimwela Limbakisye na mhandisi wa mradi huo Awariywa Nnko
kuwaruhusu wananchi kuanza kuutumia mradi huo wakati jitihada za
kuukamilisha zikiendelea
"Ndugu zingu viongozi wa wilaya ya Mufindi na mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarita Kalalu naomba kuwapongeza
San
a kwa kazi nzuri mliyoifanya katika kusimamia miradi ya maendeleo
katika Halmashauri yenu ....naomba kazi hii mzidi kuifanya kwa nguvu
Kama hizi ili kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi zaidi"
Katika
hatua nyingine Mwanri aliwataka wananchi wa Mgololo na wakazi wa wilaya
ya Mufindi kuendelea kuutumia miradi hiyo kwa kuboresha maisha yao na
kuwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete imeendelea kuboresha maisha ya
watanzania kwa kuanzisha kusogeza maendeleo mbali mbali kwa wananchi
wake.
Alisema
kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanaendelea kupinga kazi nzuri
inayofanywa na serikali ya Rais Kikwete na kuwa wananchi wasikubali
kudanganywa na wapinga maendeleo hao Kwani hawataki kuona serikali
ikiwasaidia wananchi wake ili wapate kuichafua serikali.
Akizungumzia
maofisi agani katika Halmashauri ambao wamekuwa wakishinda maofisini
walipata kiyoyozi na kuvaa suti badala ya Kwenda mashambani kwa wakulima
kuwasaidia kujua na kulima kwa kuzingatia taratibu bora za kilimo.
Hivyo
aliagiza kuanzia sasa Maofisa hao wanaowajibika kwa wakulima na
wafugaji kutoka ofisini na Kwenda kuwajibika kwa wakulima na wafugaji
katika vijiji badala ya kushinda mijini na ofisini wakishindana kuvaa
suti.
Kwa
upande wake mhandisi mradi wa umwagiliaji katika Halmashauri ya wilaya
ya Mufindi Bw.Nnko alimweleza naibu waziri huyo kuwa mradi huo wa
umwagiliaji Mgololo una zaidi ya heat 1,000 ambazo zitanufaisha kay a
1,808 zanye wakazi 7,693.
Alisema
kuwa kazi ya ujenzi wa mfereji huo wa umwagiliaji inafanywa na
mkandarasi Boimanda Modern construction co.Ltd ya mkoani Iringa chino ya
mkurugenzi wake Nicholaus Mgaya na kuwa kiasi cha zaidi ya shillingi
bilioni 1.4 zitatumika kukamilisha mradi huo.
Nnko
alisema kuwa baada ya mradi huo kukamilika hekta 700 zitalimwa na
kumwangiliwa hivyo kufanya wananchi zaidi ya 7693 wa vijiji vya Lugorofu
na Makungu kufaidika na mradi huo na kuwa mazao yatakayolimwa katika
mradi huo ni mpunga ,Mahindi ,maharage na bustani za mboga mboga.
Wakati
huo huo Mwanri ameagiza wananchi na Halmashauri za wilaya nchini
kusaidia kujenga vituo vya polisi katika vijiji na kata ili kusaidia
kupambana na wimbi la uharifu katika maeneo ya vijijini.
Alisema
kuwa uharifu umekuwa ukiendelea kutokuwa maeneo ya vijijini kutokana na
serikali kusahau kujenga vituo vya polisi katika maeneo ya kata na
hivyo kutaka wananchi na Halmashauri kushirikiana kujenga vituo vya
polisi.
Comments