Mwizi mmoja hapa London aliyekuwa akijaribu kukimbia baada ya kufanya wizi wake, aliuhisi mkono wa sheria ukimkamata baada ya kuanguka, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake katika mtindo uitwao mlegezo, au kata K.
Gazeti la Metro limesema John O'Dell alisimamishwa na polisi katika eneo la harringey, kaskazini mwa London siku ya Jumapili, lakini badala yake akaamua kukimbia.Hata hivyo, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake bila mkanda na katika mtindo wa mlegezo, suruali hiyo iliteremka na kumfanya adondoke na kukamatwa na polisi mara moja. Tukio hilo lilishuhudiwa na wapita njia. Mpita njia Harry Robbins aliyeshuhudia sakata hilo amesema, kwa kuwa hakuwa amevaa mkanda, ilikuwa ni kichekesho jinsi suruali yake mwenyewe ilivyomuangusha na kusababisha kukamatwa. Wote tuliokuwepo tulibaki tukicheka, amesema Robbins. Mwizi huyo baada ya kukamatwa alikiri kuiba laptop ya karibu dola mia tano -- atafikishwa mahakamani Januari 31.
Comments