NYETI ZA MWANAMKE ZATOWEKA USINGIZINI - MBEYA




Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Tunkumbukege Mbalaswa (20) mama wa watoto wanne mkazi wa kijiji cha Nsongola kata ya Bujela wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya amekuwa kwenye wasiwasi baada ya sehemu zake za siri kutoweka usiku wa Desemba 30 mwaka uliopita.

Akiongea kwa masikitiko Bi  Tunkumbukege amesema alijifungua salama kabisa mtoto wa kiume October 2011 aitwaye Shaban Elia na hakupatwa na tatizo lolote hadi Desemba 30, mwaka jana alipokutwa na tatizo la sehemu za siri zikiwa zimeondolewa hali iliyomsababishia maumivu makali na hivyo kumlazimu kwenda Zahanati ya Bujela na kuonana na Daktari wa zahanati hiyo na kumpata dawa mama huyo akidai ni ugonjwa wa Fistula.

Baada ya siku saba za matibabu kumalizika hali ya mwanamke huyo iliendelea kuwa mbaya huku sehemu zake za siri zikionekana zimekeketwa na tundu la mkojo kutobolewa na spoko ya baiskeli hali ambayo haja ndogo ikimtoka bila utaratibu na kupata hadha kubwa.

Bi  Tunkumbukege Mbalaswaalijifungua mtoto wa kwanza mwaka 1997, na mtoto wa pili mwaka 2003 wote wakiwa ni jinsi ya kike, mtoto wa tatu mwaka  2006 na mtoto wa kiume mwaka 2011 wote wakiwa ni jinsi ya kiume ambapo wote hajapata matatizo yoyote katika uzazi.

Kwa upande wake Mumewe Bwana Elia Mwambapa amesema matatizo yote amemwachia Mungu kwani mkewe amekuwa akipata shida licha ya kumaliza dawa, mkewa hajapata hafueni yoyote.

Uchunguzi uliofanywa na Daktari amesema katika utabibu wake hajawahi kukumbana na mgonjwa mwenye tatizo hilo  na kwamba baada ya vipimo vya Fistula amegundua kuwa mgonjwa wake hana ugonjwa huo(Fistula).

Kufuatia hali hiyo Bi Tunkumbukege anahusisha tatizo hilo na imani za kishirikina hali ambayo imepelekea kupatiwa matibabu na mganga wa tiba za asili(jadi)ambaye hakupenda kumtaja jina.

Mkoa wa Mbeya ni moja ya mikoa ambayo imekuwa ikihusishwa kutawaliwa na imani za kishirikina, hali ambayo imepelekea wakazi wake kuendelea kuishi kwa hofu, kutokana na baadhi ya watu kuendekeza kuishi katika imani hizo na wengine kuuawa na wananchi wenye hasira kali. HABARI KWA HISANI YA MBEYA YETU BLOG

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA