POLISI ARUSHA WAFANIKIWA KUUA JAMBAZI AMBAYE ALIUWA POLISI,NA KUMJERUHI MPELELEZI MKUU WA WILAYA YA ARUSHA VIJIJINI
Kamanda
wa polisi mkoa wa Arusha Thobias Angengenye akionesha moja ya silaha
ambazo zilikuwa zikitumika na jambazi huyo aliyeuwawa na polisi mapema
leo asubuhi.
Na Gladness Mushi wa Fullshangwe-ARUSHA
JESHI
LA POLISI mkoani Arusha limefanikiwa kumuua jambazi sugu ambaye wiki
iliyopita naye aliua askari na kumjerui afisa wa jeshi hilo kwa wilaya
ya arusha vijijini.
Kamanda
wa polisi mkoani hapa Thobias Angengenye alisema kuwa tukio hilo
lilitokea katika eneo la Lalashi kitongoji cha Lengine wilayani
Arumeru.
Kamanda
Andengenye alieleza kuwa katika tukio hilo jambazi huyo ambaye
alifahamika kwa jina la Pokea Samson Kaaya alikuwa alipata majeraha
katika sehemu ya mguu ambapo katika siku yatukio alikuwa akijibishana
risasi na askari polisi na hivyo akaogopa kwenda hospitalini kwa kuwa
angeweza kushikwa kwa uraisi sana.
Andengenye
alibainisha kuwa kutokana na hofu hiyo ilimfanya jambazi huyo kutafuta
mganga wa kienyeji ambapo alifanikiwa kuingia katika nyumba ya Bi Anna
Loshilari katika eneo la Orarashi.
Alisema
kuwa kuwepo kwa jambazi huyo katika eneo hilo kulifanya raia wema
waweze kutoa taarifa kwa jeshi hilo ambapo polisi walifuatlia nyendo
pamoja na taarifa hizo kwa umakini na kuweza kumpata jambazi huyo
katika eneo hilo akiwa amelala ndani hali ambayo ilifanya askari
kuzunguka nyumba hiyo hadi majira ya saa 6.45 asubui na ndipo jambazi
huyo alipotoka huku akiwa anakimbia
Kamanda
alibainisha kuwa jambazi huyo alikimbia umbali mrefu sana lakini gafla
akanza mapambano na askari kwa nia ya kuchukua silaha na kisha kuwajerui
lakini hakufanikiwa kuchukua silaha na badala yake alifanikiwa
kumjerui askari wa jeshi hilo kwa kumngata kidole gumba na lkumtoboa
jicho hali ambayo iliza mapambano makali sana ambayo yalisababisha kifo
chake hapo hapo.
Pia
alisema kuwa mara baada ya kufariki askari walifanikiwa kuwakamata
watu wanne akiwemo mke wa wa jambazi huyo pamoja na silaha ambazo nazo
zilipatikana katika eneo la Moshono ambapo silaha hizo ni pamoja na SMG
No 1016188011 , risasi kumi na moja,Shortgun
Moja yenye Model 88-12GA,risasi nne ambapo zilikuwa zimehifadhiwa katika
mfuko mkubwa wa Salphate huku zikiwa zimefichwa katika eneo la vichaka ndani ya eneo hilo la Moshono.
Comments