Senegal yabanduliwa


Kily alifunga Equitorial Guinea goli la kihistoria

Wenyeji wenza Equatorial Guinea imeshangaza wengi kwa kuibandua njee ya mashindano ya kombe la nchi bingwa barani Africa .

Kabla ya mashindano hayo kuanza , Senegal ni mojawapo ya nchi ambazo zilikuwa zimepigiwa upato wa kushinda kombe hilo.

Lakini Equatorial Guinea ambayo katika nafasi ya 151 katika orodha ya FIFA ya hivi karibuni waliyakatiza mautumaini ya Senegal.

Aliyefungua ukurasa wa magoli ni Randy lakini katika dakika ya 89 Moussa Sow aliifngia Senegal bao na kufanya mambo kuwa 1-1.

Ni katika dakika za majeruhi ambapo mchezaji Kily alifumua mkwaju mkali toka umbali wa yadi 25 hadi kimyani. Hivi mambo ya kawa Equitorial Guinea 2 Senegal 1.

Japo matokeo hayo ni pigo kwa Senegal lakini ni furaha kwa timu ya Newcastle ya Uingereza kwani washambulizi wake Demba Ba na Papiss Cisse wanarudi uingereza kuisaidia timu yao katika mechi za Premier.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA