Vodacom Foundation yakabidhi madarasa 3 na madawati 100 S/Msingi Ruvu Darajani

Ofisa Mkuu wa masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba kushoto akipokea zawadi ya mbuzi toka kwa baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo mkoani pwani,mara baada ya kuwakabidhi rasmi vyumba vitatu vya madarasa na madawati 100 kwa ajili ya shule hiyo,Msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 98.
Haya ndiyo madarasa ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani yaliyojengwa na Vodacom Foundation.
Mkurugenzi wa Wizara ya Elimu shule za Msingi,Zuberi Samataba mwenye suti akiongea jambo na 0fisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,walipowasili katika shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani kwa ajili ya kukabidhi msaada wa madarasa matatu na madawati 100 uliotolewa na Vodacom Foundation katika shule hiyo na kugharimu zaidi ya shilingi Milioni 98.
Hili ndilo jiko la wanafunzi wa shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani,Taswira hii imepigwa na mpiga picha wetu katika makabidhiano ya vyumba vitatu vya madarasa pamoja na madawati 100 vilivyokabidhiwa rasmi mwishoni mwa wiki na Vodacom Foundation kwa ajili ya shule hiyo,wadau jitokezeni msaidie hata kujenga jiko hilo.
Kikundi cha ngoma cha wazazi wa mkoa wa Pwani wakitumbuiza wakati wa makabidhiano rasmi wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na madawati 100 vilivyokabidhiwa rasmi mwishoni mwa wiki na Vodacom Foundation kwa ajili ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani,Msaada huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 98,
0fisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na madawati 100 vilivyokabidhiwa rasmi na Vodacom Foundation kwa ajili ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani,Msaada huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 98,kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa shule za msingi Wilaya ya Bagamoyo na kushoto ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Mary Nzowa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.