WAFUNGWA JELA KWA KUTOMLILIA KIM JONG IL

Mazishi ya Kim Jong-il
Mamlaka za Korea kaskazini zinadaiwa kuwaadhibu wananchi wake kwa kuwapeleka jela na kazi ngumu-- wale wote ambao hawakulia vya kutosha katika msiba wa kiongozi wao Kim Jong-il.
Gazeti la kila siku lenye makao yake makuu Korea Kusini NK limesema yeyote ambaye hakushiriki misa ya kihistoria ya kumuenzi Kim au ambaye alihudhuria lakini hakulia kiasi cha kutosha au kuonekana kulia kwa uongo, atapelekwa katika kambi maalum na kufanyishwa kazi ngumu kwa miezi sita, limeripoti gazeti hilo.
Gazeti hilo limedai huku likikariri chanzo ambacho haikukitaja kuwa yeyote aliyejaribu kutoka nje ya nchi wakati huo atashtakiwa katika mahakama mbele ya kadamnasi. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa kwenye mtandao wa cnews.com, wengine watapelekwa katika kambi na kupewa elimu upya ya utaifa.
Hakuna taarifa rasmi kutoka Korea kaskazini iliyothibitisha taarifa hizi. Hata hivyo shirika la habari la Korea Kaskazini limeripoti wiki iliyopita kuwa kifo cha Kim Jong-il kiliombolezwa hadi na wanyama wa porini.
"Dubu mmoja akiwa na wanae walionekana wakiwa wanalia kwa nguvu" imesema taarifa ya shirika hilo. Madubu hao sio wanyama pekee ambao wameripotiwa kumuomboleza kiongozi huyo.
Shirika hilo liliripoti mwezi uliopita kuwa mamia ya kunguru aina ya Magpies walionekana wakipeperuka kuzunguka sanamu la Rais Kim katika wilaya ya Magyondae.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA