WEMA AMZODOA DIAMOND MCHANA KWEUPEE..!!

Hatimaye mrembo na msanii Wema Sepetu, ameweka wazi kuwa hataki tena kutembea na masharobaro kwani mapenzi yao yanakuwa hayana malengo zaidi ya kuchezeana.

Akizungumza hivi karibuni msanii huyu alisema kuwa msanii anayemfananisha na sharobaro ni aliyekuwa mpenzi wake
Nassib Abdul ‘Diamond’, kwani endapo angekuwa hayuko hivyo basi anaamini mapenzi yao yangedumu kwa muda mrefu.

Alisema kwa sasa anahitaji kutoka na mwanaume aliyemzidi umri kwani anaamini watu hao wanakuwa na mapenzi ya dhati tena hawana wivu kama watoto wadogo ambao muda wote hupenda kuwa karibu na wapenzi wao badala ya kufanya kazi.


“Kila kitu kina muelekeo wake, mapenzi yangu mimi na Diamond yangeweza kudumu lakini kutokana na usharobaro alionao ndiyo uliosababisha yote yaliyotokea, na ndiyo maana nasema kwamba ni bora kutembea na mwanaume aliyekuzidi umri mnaweza kufika mbali,”
alisema.

Msanii huyu alisema hata hivyo ni bora afunge ndoa na mwanaume atakayempata ambaye anajua maana ya mapenzi kuliko kutembea na vijana wadogo ambao hawajui nini maana ya mapenzi na hawana muelekeo wa maisha.CHANZO BLOG YA UNIQUE

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA