EU YAIONDOLEA VIKWAZO ZIMBABWE

Muungano wa Ulaya umewaondolea vikwazo baadhi ya maafisa wakuu wa serikali ya Zimbabwe, ingawa utaendelea kushikilia mali ya rais wa nchi hiyo Robert Mugabe pamoja na washirika wake wa karibu.

Kwa mujibu wa muungano huo, vikwazo vya usafiri dhidi ya mawaziri wawili viliondolewa ili kushinikiza serikali kuharakisha mchakato wa mageuzi.

Lakini msemaji wa chama cha rais Robert Mugabe,alipinga hatua hiyo akitaja vikwazo hivyo kama vinavyokiuka sheria, vyenye misingi ya ubaguzi wa rangi na vitakavyoathiri uchumi wa nchi.

Muungano huo pia uliondoa takriban kampuni ishirini za serikali kwenye orodha hiyo ambazo muungano huo ulidai kuwa zilisaidia kufadhili vurugu nchini Zimbabwe.

Ingawa Zimbabwe imepiga hatua katika mchakato wa kuunda katiba mpya, na kuimarisha uchumi, Muungano huo ungali na wasiwasi ikiwa ahadi zilizowekwa baada ya uchaguzi uliokumbwa na vurugu mwaka 2008, ikiwemo ahadi za kufanyia mabadiliko idara ya polisi hazijaweza kutimizwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*