Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Angetile Osiah ameondoka juzi kwenda nchini India kufanyiwa upasuaji wa kichwa katika Hospitali ya Apollo.
Osiah hivi karibuni alilazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kitengo cha Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI), ambapo alilazwa kwa kusumbuliwa na uvimbe kichwani.
Upasuaji huo umetokana na ushauri wa madaktari waliokuwa wana mpatia matibabu katika Taasisi hiyo.
Uongozi wa Blog ya Kamanda wa Matukio unamtakia matibabu mema na unaamini kuwa Mungu atamjalia, Amina.
Comments