Kimbunga chaathiri Madagascar

Kimbunga chenye upepo mkali wa mwendo wa kilomita 194 kwa saa kimeathiri kisiwa cha Madagascar kwa kung'oa miti na vifaa vya kusafirisha umeme.

Kimbunga hicho, ambacho kimepewa jina Giovanna kilianza kwa kuathiri mji wa Toamasina, mashariki mwa kisiwa hicho.

Magari ya huduma za dharura yameonekana jijini Antananarivo yakiondoa vifusi.

Wataalam wa masuala ya hali ya hewa wanaonya kwamba uharibifu katika kisiwa hicho huenda ukawa mbaya kama ule wa 1994 , wakati kimbunga kilipowaua watu 200 na kuwaacha wengine 40,000 bila makaazi.

Afisa mmoja wa serikali ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba Takriban mtu mmoja amefariki dunia katika mji wa Brickaville baada ya kuangukiwa na nguzo ya umeme.

Watu wamebakia majumbani mwao kwa sababu ofisi, shule na biashara zimefungwa na umeme umekatika.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI