MAKAMU WA RAIS WA CHINA AWASILI MAREKANI

Makamu wa Rais wa Uchina, Xi Jinping, ambaye anatarajiwa kuwa kiongozi wa juu wa nchi baadaye mwaka huu, amewasili nchini Marekani akiwa katika ziara rasmi.

Anatarajiwa kukutana na Rais Barack Obama katika Ikulu ya nchi hiyo baadaye leo, kujadiliana masuala mbalimbali yenye msuguano kati ya nchi mbili hizo.

Miongoni mwa masuala hayo ni mvutano kuhusu Syria, Iran na Korea Kaskazini, uimarishaji wa majeshi katika Asia Mashariki na nakisi kubwa ya kibiashara ya Marekani na Uchina.

Bwana Xi anaonekana kuwa ndiye atakayechukua uongozi wa Chama cha Kikomunisti katika mkutano mkuu wa chama hicho utakaofanyika Beijing mwishoni mwa mwaka huu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA