MKUTANO WA KAMATI YA UTENDAJI YA CPA KANDA YA AFRIKA, WAANZA ARUSHA
Naibu Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akijadili jambo na Spika wa Bunge la Afrika Kusini Mhe. Mninwa Mahalangu (Mb) ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Utendaji CPA Afrika alipofika nchini kuhudhuria Mkutano wa siku moja wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA Africa) unaofanyika mjini Arusha tarehe 25 Februari, 2012. Picha na Owen Mwandumbya
Naibu Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akimkaribisha Spika wa Bunge la Rwanda Mhe. Rose Mukantabana (Mb) Mjini Arusha jana, mara alipofika nchini kuhudhuria Mkutano wa siku moja wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA Africa) unaofanyika mjini Arusha tarehe 24 Februari, 2012. Mhe. Rose Mukandabana ni Rais wa Chama hicho kwa kanda ya Afrika. Picha na Owen Mwandumbya
Wajumbe wa sekretariati ya Chama cha Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA Africa), wakiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya chama hicho kilichofanyika mjini Arusha februari, 25, 2012. Kutoka kulia ni Dk. Thomas Kashililah, Katibu wa Kanda wa chama hicho ambae pia ni katibu wa Bunge la Tanzania, Demetrius Mgalami, Naibu katibu wa CPA Afrika na Said Yakubu Mjumbe wa Sekretariat ya CPA Afrika. Picha na Owen Mwandumbya
Katibu wa Chama cha Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA Africa) Dk. Thomas Kashililah ambaye pia ni katibu wa Bunge la Tanzania akifafanua jambo kwa Spika wa Bunge la Afrika Kusini Mhe. Mninwa Mahalangu (Mb) (Kulia) ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Utendaji CPA Afrika wakati wa kikao cha kamati ya Uongozi ya chama hicho iliyokutana Mjini Arusha, leo. Picha na Owen Mwandumbya
Comments