ONYESHO LA LADY IN RED RELOADED 2012 LAFANA SANA SERENA HOTEL DAR ES SALAAM USIKU HUU
Mwandaaji wa onyesho la mavazi la 'Lady in Red' Reloaded 2012 Asia Idarous akiwa katika picha ya pamoja na mume wake Bw. Wa Hamsini katika onyesho hilo lilinalofanyika usiku huu kwenye hoteli ya Serenea Dar es salaam jijini Dar es salaam, onyesho hilo pia litatumika kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga kituo cha kuhudumia watu walioathirika na madawa ya Kulevya hapa nchini. kitakachojengwa huko Kikale, Rufiji mkoani Pwani
Mmoja wa wanamitindo akipita na moja ya mavazi yaliyobuniwa kwa ajili ya siku ya wapendanao katika onyesho la mavazi la Lady In Red jijini Dar es salaam.
Mshereheshaji wa onyesho hilo akitoa ratiba ya onyesho hilo siku huu katika hoteli ya Serena Dar es salaam.
Mtangazaji wa Clouds TV akifanya mahojiano na warembo wa zamani Jaquiline Patrick na mrembo Lisa Jensen katika onyesho hilo.
Comments